Monday, October 29, 2012

LEXA MMOJA WA WATENGWA ACHOMWA KISU NA KUFARIKI


Juzi ijumaa ya tarehe 26 october nilipokea sms nyingi zikinitaka kufafanua na wengine kuniuliza kama habari zinazohusu kifo cha memba wa atengwa anaeitwa Lexa ni kweli ama si kweli..sasa kwa habari nilizonazo ni kuwa info hizo ni za kweli na ilitokea siku ya ijumaa ambapo alikabwa na kunyang'anywa vitu vyake na watu wanaomfaham na kisha kumchomwa kisu..zaidi msikilize Ben mmoja kati ya wanaounda kundi la waturutumbi

"nikweli jamaa amededi kweli , maana jamaa walimkaba wakamuibia mavitu yake nini lakini wanamjua yaani ni watu tunakaa yaani pamoja yaani, kuna machalioi ambao wanamjua mmoja walimshika jana bado wawili naskia ndio wanatafuta...Jcb mara ya mwisho ndio alikua nae so lazima uchunguzi uendelee..." amesema mmoja lakini baadae JCB aliandika kupitia ukurasa wake wa facebook kuhusu ishu hiyo

Jcb Makalla
Tarehe 26 ijumaa hii sitaisahau maishani mwangu ni siku niliyo mpoteza rafiki yangu kipenzi lexa julias,na mimi nilikuwa polisi kuwasaidia kwa uchunguzi na mungu amesaidia watuhumiwa wameshikwa na wako ndani sasa,tuungane katika kipindi hichi kigumu sasa mungu amrehemu marehemu,pia naomba mungu awe karibu na familia yake kwa hichi kipindi kigumu,rest in peace my best friend lexa..amen
Lexa anafikisha idadi ya watengwa watatu wliofariki kwa beto, akiwemi Father Nelly, Pacha aliechomwa kisu na malaya na Lexa
tatizo ni nini Arusha!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Kunani Chugaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!!
















HIVI NDIO VICHWA VYA HABARI YA MAGAZETI YA LEO, KWANZIA LEO TUTAKUA TUNAWALETEA VICHWA VYA HABARI MAGAZITINI KWA MAJARIBIO YA BLOG HII


widgets

SPORTS NEWS