MTAFUTAJI BLOG

Pages

  • Home
  • HARDWARES
  • IT TECHNICS
  • MATOKEO YA FORM 4, 2012
  • SPORTS

Tuesday, February 26, 2013

CHADEMA: Kawambwa amebakiza siku kumi

 

KAULI ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa kwamba hawezi kujiuzulu, imeamsha hasira ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ambacho kimesisitiza kwamba maandamano ya kumng’oa yako pale pale na sasa amebakiza siku kumi. Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkurugenzi wa Habari na Uenezi, John Mnyika wakati alipotakiwa kueleza msimamo wa chama chao, hasa baada ya kauli ya Waziri Kawambwa jana kwamba hawezi kujiuzulu.

Read more »
Posted by Unknown at 1:25 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Waraka wa Tatu wa Lema Kwa Rais Kikwete

Mh Rais Nakusalimu .

Wakati mwingine unapaswa kupewa pole na kuombewa na kufanyiwa dua kwani wewe ndie unatumikia ofisi kubwa kuliko zote Nchini na wakati huo huo unapaswa kupewa hongera kufikia malengo yako hayo ya kutumikia ofisi kubwa na ya Heshima kuliko zote Nchini , nimekuwa nikitafakari sana suala la Udini katika Taifa letu na huko Nyuma mwaka jana nilikuandikia pia waraka kuonya na kukumbusha hatua mathubuti kabla mambo hayajaaribika sijui kama ulisoma lakini naamini Usalama wa Taifa ambao siku hizi wanatumikia CCM watakuwa walisoma na Nape na wenzake pia walipata fursa ya kuusoma .


Read more »
Posted by Unknown at 12:58 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Saturday, February 23, 2013

Zanzibar: Imamu wa msikiti auwawa kikatili!

 Na Mohammed Mhina, wa Jeshi la Polisi - Zanzibar


Mzee mmoja mkazi wa Kitopeni mkoa wa Kaskazini Unguja Zanzibar Bw. Ali Khamis Ali (65), ameuawa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali shingoni na watu wasiojulikana.

Read more »
Posted by Unknown at 8:51 PM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

DEMU MPYA WA DIAMOND WAMFANANISHA NA WEMA.



Avril Nyambura.
 IMEBAINIKA kuwa, mwanamuziki ambaye aliwahi kudaiwa kutoka kimapenzi na Nasibu Abdul ‘Platnumz’, Avril Nyambura ni staa anayetingisha kwa skendo nchini Kenya lakini anapendwa ile mbaya. 
Chanzo cha habari ambacho kinaishi nchini Kenya kililiambia Ijumaa hivi karibuni kuwa, Avril kwa skendo anatisha lakini cha ajabu ni staa wa kike anayewavutia wengi nchini humo.

 “Yaani Avril ni kama Wema wa Kenya, anatisha kwa skendo, kila siku magazeti yanamuandika na hivi karibuni aliandamwa na ishu ya usagaji, cha ajabu anapendwa sana. Yaani ni kama ilivyo kwa Wema wa Tanzania,” alisema mdau huyo.
Posted by Unknown at 9:43 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

MNYIKA VS NAPE, FORM FOUR RESULTS NAPE NNAUYE

MNYIKA VS NAPE, FORM FOUR RESULTS
NAPE NNAUYE

DIV IV-29
KISW D, HIST D, GEOG D, ENG F, B/MATH F, BIOL D, CHEM D, PHY D, CIV
JOHN MNYIKA
DIV I-7
PHY A, CHEM A, BIOL A, CIV A, ENGL A, GEOG A, HIST A, B/MATH A, KISW A, B/KNOW A

MY TAKE: MNYIKA NI GINIAZI
NAPE AJIENDELEZE
Ref; Jay Chadema
— with Chadema Bunda and 44 others.
Posted by Unknown at 8:13 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Patrice Muamba uanjani tena




Yule mchezaji mahiri aliekua akikiputa kwenye timu ya bolton Wanderers alielazimishwa kustaafu baada ya kuangua kuanjani kwa tatito la moyo kusimama kwa muda wa masaa 78.

Jumapili hii atakua katika uanja wa taifa wembley akikabizi kombe kwa mshindi wa kombe la ligi


Posted by Unknown at 8:04 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Friday, February 22, 2013

BEKI BLACK STARS (John Paintsil) AMEMSHAMBULIA MKEWE NA KUMJERUHI VIBAYA



 

Mlinzi wa Black stars(Ghana) amekamatwa na yupo chini ya pilice kwa kosa la kumjerui mkewe.
Taarifa hili imetolewa na kituo cha police cha mjini Accra, Greater Accra Police PRO Freeman Tettey kwenye intaview aliofanya na Joy News Muda mfupi uliopita.
Ilikiri kua ukweli bado haujajulikana ila sababu zilizopelekea kufanya hivyo na kutoelewana kati ya John na mkewe.
Taarifa ya mwandishi  Haruna Maiga alioko maeneo ya Legon police ambopo John Paintsil ameshikiliwa anasema kua John aliletwa police hapo akiwa na watoto wake watatu akiwa na kundi la police kama escot ya kumfikisha kituo cha police
Katika taarifa ya mwanzo katika jalada la police linasemakana John ameandikiwa makosa mawili kua amefanya shambulio na kutoa lugha chafu ya matusi kwa mkewe.

Mkewe, Richlove Paintsil aliruka ukuta wa nyuma yao na kuingia kwa nyumba ya jirani kujinusuru na ugomvi uliokua ukirindima ndani ya nyumba yao dhidi yake na mumewe John.
Richlove amejeruhiwa vibaya maeneo ya jicho na mumewe.
Ugomvi wote huo ulisababishwa na skendo zilizokua zikivuma kuhusu John kua alikua anatoka nje ya kambi kipindi cha kombe AFCON 2013 nnchi africa ya kusini kuwaletea wenzake wanawake wakustarehe nao ambayo ilipekea Black Stars kufanya vibaya
katika mashindano hayo skata hilo lilianzishwa na shabiki mmoja ambae pia ni mtangazaji wa redio Nnchi humo





Posted by Unknown at 10:45 PM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Kanisa katoliki laruhusu tembe za kuzuia mimba


Kanisa Katoliki nchini Ujerumani limeamua kuwa ni halali kwa mwanamke kutumia tembe ya kuzuia mimba mara tu baada ya kubakwa.

 

 Tembe za kuzuia mimba

Uamuzi huu umefanywa kufuatia mkutano wa viongozi wa Kanisa Katoliki nchini Ujerumani baada ya mwanamke mmoja aliyekuwa amebakwa kusema kuwa alizuiwa kufanyiwa matibabu siku mbili mfululizo katika Hospitali zinazofadhiliwa na Kanisa Katoloki zikisema kuwa kuzima mimba ni kinyume cha maongozi yake.

Read more »
Posted by Unknown at 4:33 PM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Kanisa katoliki laruhusu tembe za kuzuia mimba


Posted by Unknown at 4:29 PM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

JCB Afunga Ndoa...






Rapper kutoka kundi la Watengwa lililopo A-City, JCB ambae hivi karibuni ametoka kuachia track yake inayokwenda kwa jina la Niende Wapi akiwa ameshirikiana na Domokaya amevuta jiko hivi karibuni...

JCB sasa ameuacha u-bachelor rasmi baada ya kufunga ndoa rasmi siku ya jumatano ya Tarehe 20 mwezi huu. Ndoa hii imeonekana kuwa ni ya kimya kimya sana maana sio watu wengi waliokuwa wakijua juu ya tukio hilo.
Hizi ni baadhi ya picha za kwenye harusi hiyo...







Posted by Unknown at 4:19 PM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Diamond Platnumz Azungumzia Kuhusu Mganga Aliyejitokeza...


 Hivi karibuni, alijitokeza mganga wa kienyeji akidai kumfanyia Diamond Platnumz dawa za kienyeji za ziada ili aweze kuwa na nyota nzuri kwenye muziki na kung'ara kama alivyo sasa.

Mganga huyo alikwenda katika moja ya magazeti ya udaku ya hapa nchini na kudai, Platnumz amekuwa hapokei simu zake hasa baada ya kufanikiwa katika muziki na maisha yake kiujumla huku haikuwa hivyo kipindi cha mwanzo.

Diamond alikuwa kimya na muda mrefu na mara kwa mara amekuwa akikanusha habari hizi kuwa si za kweli na kusema hamjui mganga huyo na kuwa yeye hashiriki vitu kama hivyo.

Lakini hivi karibuni Diamond ameamua kuongea ukweli hasa pale alipofanya interview a kituo kimoja cha Redio cha hapa jijini Dar na kuzungumza almost kila kitu kuhusu suala hili.



Msikilize Mr. Diamonds akiongea hapa chini:

Bofya Hapa
Posted by Unknown at 4:10 PM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Wanafunzi wajiua kwa matokeo kidato cha IV


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Anthony Rutta

Matokeo mabaya ya mtihani wa taifa wa kumaliza kidato cha nne wa mwaka 2012 yamesababisha maafa baada ya wahitimu wawili waliofeli kujinyonga.
Wahitimu waliojinyonga katika matukio mawili tofauti ni wa mikoa ya Tabora na Dar es Salaam.

Katika tukio la kwanza, mhitimu katika Shule ya Sekondari ya Kanyenye mjini Tabora ambaye ni mkazi wa Mtaa wa Mwinyi Kata ya Chemchem, Manispaa ya Tabora, Michael Fidelis (19), amejinyonga.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Anthony Rutta, alisema mwanafuzi huyo alikwenda kuangalia matokeo Jumatatu saa 11:00 jioni huu na baadaye alikutwa amejinyonga hadi kufa chumbani kwake kwa kutumia kamba ya manila.
Kamanda Rutta alieleza kuwa marehemu alipata daraja la sifuri na kwamba aliacha ujumbe uliosomeka: “Nisamehe sana mama usitafute mchawi, nakupenda sana, uamuzi niliouchukua ni sababu ya matokeo mabaya, nakutakia maisha mema.”

Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kenyenye, Kapufi Patson, alisema kuwa mwanafunzi huyo alikuwa ni mpole na mtaratibu na wameshangazwa na uamuzi aliouchukua wa kujinyonga.
Matokeo ya shule hiyo yanaonyesha hakuna mwanafuzi aliyepata daraja la kwanza wala la pili isipokuwa waliopata daraja la tatu ni wawili, la nne ni 14 na waliopata sifuri ni 85. Wahitimu 36 matokeo yao yameuiliwa kwa sababu ya kudaiwa ada ya mtihani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Engelbert Kiondo


ALIYEJINYONGA DAR
Katika tukio la pili, mhitimu katika Shule ya Sekondari Debrabant iliyopo Mbagala, wilayani Temeke jijini Dar es Salaam, Barnabas Venant (18), amejinyonga kutokana na matokeo mabaya.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Engelbert Kiondo, alisema jana kuwa kijana huyo, mkazi wa Nzasa, alikutwa amejinyonga kwa kamba aina ya manila ndani ya stoo ya nyumba yao.

Kamanda Kiondo alisema, tukio hilo lilitokea juzi saa 10:00 jioni baada ya kijana huyo kutoridhishwa na matokeo ya mtihani huo ambayo alipata daraja la nne, tofauti na matarajio yake.
Alisema uchunguzi wa tukio hilo unaendelea na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Temeke.

HAKIELIMU YAKOSOA


Wakati huo huo, serikali imelaumiwa kuwa ndiyo chanzo cha matokeo mabaya ya mtihani wa kidato cha nne uliofanyika mwaka jana, kutokana na kutotumia tafiti na mapendekezo mengi ambayo yamekuwa yakitolewa na asasi mbalimbali na wataalamu.

Aidha, imepewa angalizo kuwa wanafunzi watakachaguliwa kujiunga na kidato cha tano, wawe ni wale waliofaulu bila ya kutumia kigezo cha kuchagua hata wanafunzi waliopata daraja la nne kwa nia ya kujaza nafasi za kidato cha tano kama ilivyofanya kwa waliojiunga na kidato cha kwanza mwaka 2013.

Kauli hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Elizabeth Missokia, Mkurugenzi Mtendaji wa HakiElimu kupitia tamko kwa vyombo vya habari kuhusiana na matokeo ya kidato cha nne.

Missokia alisema HakiElimu walianza kuitahadharisha serikali na jamii kuhusiana na hali mbaya tangu mwaka 2010, baada ya asilimia 49 ya wanafunzi waliofanya mtihani kidato cha nne kupata daraja sifuri.

“Tulitoa angalizo kuwa kama juhudi za makusudi kuboresha ufundishaji na ujifunzaji hazitafanyika, basi tutarajie idadi kubwa ya wanafunzi kufeli miaka ijayo na ndicho kimetokea kwani tumeanza kuvuna tulichopanda,” alisema.

Missokia aliwaasa wananchi kuhakikisha kwamba serikali haiendelei kubahatisha katika suala la utoaji wa elimu kwa kuwa wana wajibu wa kuishinikiza kwenye suala la utoaji wa elimu bora kwa watoto wa Kitanzania kwa mustakabali wa taifa.

Akizungumzia watakaochaguliwa kujiunga na kidato cha tano, Missokia alisema kwa kuangalia matokeo ni dhahiri kwamba wanafunzi takribani 23,520 kati ya 367,750 waliofanya mtihani, ndiyo wanaostahili kujiunga na kidato hicho.

Alisema wanafunzi hao 23,520 wamepata kati ya daraja la kwanza na la tatu ambayo ni asilimia sita tu ya waliofanya mtihani.

“Serikali isirudie kuchukua hata wale ambao hawakufaulu kama ilivyokuwa kwa waliojiunga na kidato cha kwanza mwaka huu, ilipoamua kuchukua wanafunzi wenye alama chini ya 100 kati ya 250, uamuzi ulioonyesha dhahiri kukosa msimamo,” alisema.

Aliitaka serikali kutambua kuwa viwango vya udhahili kwa ngazi yoyote ile ya elimu hasa ufaulu, vina mantiki ya pekee kumuwezesha mwanafunzi kumudu masomo katika ngazi anayodahiliwa.

Alisema kitendo cha kuendelea kudahili wanafunzi ambao hawana sifa ni kuendelea kupeleka wanafunzi ngazi za juu za elimu, wakati hawana uwezo wa kuyamudu masomo katika ngazi hiyo.

Pia alisema HakiElimu imeshangazwa na sababu zilizotolewa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, kuwa ukosefu wa walimu na maabara ulichangia wanafunzi wengi kufeli.

Missokia alisema kuwa kati ya mwaka 2006 hadi 2009, ikama ya walimu sekondari ilikuwa mwalimu mmoja kwa wanafunzi 50 hadi 55, na kwamba ikama ya sasa ni ya mwalimu mmoja kwa wanafunzi kati ya 35-38, hali inayoonyesha kuvuka kiwango kinachotakiwa cha mwalimu mmoja kwa wanafunzi 40.

“Pia shule nyingi hazikuwa na maabara wakati huo kuliko sasa, lakini wanafunzi waliofeli sasa wamezidi kuongezeka na kufikia asilimia takribani 61. Kwa hiyo hali hii haihitaji majibu au sababu nyepesi alizozitaja waziri,” alisema.

Alitaka kuwapo mjadala wa kina kwa wananchi na wabunge kuishikiza serikali kutambua kuwa mfumo wetu hauko sawa na kubainisha changamoto za kuurekebisha haraka kupunguza athari zitakazolikumba taifa hili na mustakabali wa elimu.




CHANZO: NIPASHE

Posted by Unknown at 7:19 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Mchungaji Antony Lusekelo azungumzia Kuchinja!

Namsikiliza Mchungaji Antony Lusekelo Chanel Ten sasa hivi.

Nimemkubali huyu kweli ni kiongozi sahihi katika Imani ya Kikristo. Tukiwa na Viongozi wa kama hawa Amani yetu ya inchi haiwezi kutetereka.

Heshima kwako Mchungaji. Natamani Wachungaji, Mapdre na Maaskofu pamoja na Makidanali wote Muwe na upeo mkubwa wa kufikiria kama huyu Mchungaji. Huyu ni Tunu ya nchi.


Kwa ufupi tu, Mchungaji Antony Lusekelo Ameshangaa kulikoni leo Mashekhe na Maaskofu au Mapadre au Wachungaji wagombane wakati waliishi kwa amani tangu zamani. Kama ni suala la kuchinja, mbona suala hilo tangu enzi ya wazee wetu, walikua wanachinja waislamu wanakula wote. "Kama tukichinja sisi waislamu hawali, basi wachinje waislamu tule wote. Kuchinja isiwe ndio sababu ya kuvunja amani ya nchi yetu".

Ameeleza kwa kirefu suala hilo. Hiyo ndio ilikua mada ya kipindi.

Huyu nimekua nikifuatilia mahubiri yake, huyu kweli anawakilisha imani sahihi ya kikristo. Mimi sio Mkristo mimi ni Muislamu, ila hua tuna wapenda viongozi kama hawa katika jamii. Sio vizuri sisi watanzania kutengana kimisingi ya dini. Ni vibaya na hatari sana. Familia nyingi ni mchanganyiko.



Posted by Unknown at 6:40 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

HATIMAE WIZ KHALIFA NA AMBA ROSE WAPATA MWANA

ILIKUA HIVI KWENYE MITANDAO KIBAO YA KIJAMII

Wiz Khalifa and Amber Rose Welcome Their First Child

IKIFWATIWA NA BO BO BONGEE LA PIC YA JAMAA AKIWA PANDE ZILEE

Haikuishi hapo, kitu kihapen kama jamaa amechangamka nane kwenye twitter pale alipotupia kama hivo hapo chini "Daddy Time" Then akatupia mpaka jina .... 

endelea

"Happy Birthday Sebastian "The Bash" Taylor Thomaz!!! ?????? Everyone welcome this perfect young man into the world"
Wiz Khalifa (@wizkhalifa

Kama vipi endelea kucheki twitter account yake ujionee mwenyewe

https://twitter.com/wizkhalifa/status/304714560563208192

Nae Amber Rose hakubaki nyuma nae alitokelezea na twit yake kuhusu furaha ya kumpata mtoto wao mpendwa "The Bash|"

Posted by Unknown at 6:19 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Tuesday, February 19, 2013

NECTA yatangaza Matokeo ya Kidato cha Nne 2012 Wakubwa, NECTA wametangaza matokeo tayari. Tembelea

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2012 - (Hosted by Mtafutaji)
Posted by Unknown at 5:22 AM 1 comment:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Monday, February 18, 2013


 







 Click Hapo chini uangalie moja kwa moja kupitia hizo link hapo


f LINK-01: MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2012 
f LINK-02: MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2012
 f LINK-03: MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2012
Posted by Unknown at 7:24 PM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
Labels: Links za kuangalia matokeo

Matokeo ya kidato cha Nne 2012

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa (MB) leo ametangaza rasmi matokeo ya Mitihani ya Kidato cha Nne, maarifa-QT.
---------------
TAARIFA YA MATOKEO YA MITIHANI YA MAARIFA (QT) NA KIDATO CHA NNE (CSEE)
ILIYOFANYIKA OKTOBA 2012
---------------------
1.0                 UTANGULIZI
Mitihani ya Kidato cha Nne (CSEE) na Maarifa (QT) kwa mwaka 2012 ilifanyika nchini kote kuanzia tarehe 8-25 Oktoba 2012.  Napenda kuchukua nafasi hii kutangaza rasmi matokeo ya mitihani hiyo kama ifuatavyo :
2.0                 MTIHANI WA MAARIFA (QT)
2.1           Usajili na Mahudhurio
Katika Mtihani wa Maarifa 2012 watahiniwa waliosajiliwa ni 21,310 ambapo wasichana walikuwa ni 13,134 na wavulana ni 8,176. 
Jumla ya watahiniwa 17,137 sawa na asilimia 80.42 ya waliosajiliwa wamefanya Mtihani. 
2.2          Matokeo ya Mtihani wa Maarifa (QT)
Watahiniwa 5,984 kati ya 17,137 waliofanya mtihani wamefaulu Mtihani wa Maarifa (QT).
3.0                 MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2012
Jumla ya vituo 5,058 vilitumika katika kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2012 ambapo vituo 4,155 vilikuwa vya watahiniwa wa shule na vituo 903 vilikuwa ni vya watahiniwa wa kujitegemea.
3.1                 Usajili na Mahudhurio ya Watahiniwa
(a)           Watahiniwa Wote
Jumla ya watahiniwa 480,036 walisajiliwa kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2012 wakiwemo wasichana 217,583 sawa na asilimia 45.33 na wavulana 262,453 sawa na asilimia 54.67.  Watahiniwa waliofanya mtihani wa Kidato cha Nne 2012  ni 456,137 sawa na asilimia 95.44. Watahiniwa 21,820 sawa na asilimia 4.55 ya watahiniwa wote waliosajiliwa hawakufanya mtihani.
(b)            Watahiniwa wa Shule
Watahiniwa wa shule waliosajiliwa ni 411,230 wakiwemo wasichana 182,978 sawa na asilimia 44.50 na wavulana 228,252 sawa na asilimia 55.50.  Watahiniwa wa shule waliofanya mtihani walikuwa 397,136 sawa na asilimia 96.57. Aidha, watahiniwa 14,090 sawa na asilimia 3.43 hawakufanya mtihani kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo utoro,  ugonjwa na vifo.
(c)             Watahiniwa wa Kujitegemea
Watahiniwa wa kujitegemea waliosajiliwa walikuwa ni 68,806 wakiwemo wasichana 34,605 sawa na asilimia 50.29 na wavulana 34,201 sawa na asilimia 49.71. Watahiniwa 61,001 wakiwemo wasichana 30,917 na wavulana 30,084  wamefanya mtihani wakati watahiniwa 7,730 sawa na asilimia 11.23  hawakufanya mtihani.
4.0                 MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE
(a)                 Watahiniwa wa Shule
Jumla ya watahiniwa wa shule 126,847 kati ya watahiniwa 397,136 waliofanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2012 wamefaulu. Wasichana waliofaulu ni 46,161 na wavulana ni 80,686.
(b)                Watahiniwa wa Kujitegemea
Idadi ya watahiniwa wa kujitegemea waliofaulu mtihani ni 16,112 kati ya watahiniwa 61,001 waliofanya mtihani.  Wasichana waliofaulu ni 6,751 na wavulana ni 9,361. 
5.0                 UBORA WA UFAULU KWA MADARAJA NA JINSI
Ubora wa ufaulu kwa kuangalia madaraja waliyopata watahiniwa wa shule unaonesha kuwa jumla ya watahiniwa 23,520 wamefaulu katika madaraja I – III ambapo kati yao wasichana ni 7,178 na wavulana ni 16,342.
Mchanganuo wa ufaulu kwa kila Daraja kwa jinsi kwa Watahiniwa wa Shule mwaka 2012 ni kama ifuatavyo:
Daraja
Idadi ya Wavulana      
Idadi ya  Wasichana
Jumla
I
1,073
568
1,641
II
4,456
1,997
6,453
III
10,813
4,613
15,426
I-III
16,342
7,178
23,520
IV
64,344
38,983
103,327
0
120,664
120,239
240,903
6.0        SHULE ISHIRINI ZILIZOFANYA VIZURI ZAIDI KATIKA KUNDI LA SHULE ZENYE WATAHINIWA 40 AU ZAIDI
------------
Ubora wa ufaulu wa shule umepangwa kwa kutumia kigezo cha “Grade Point Average” (GPA) kuanzia A = 1 hadi F = 5.  Shule zenye watahiniwa 40 na zaidi ziko 3,391. Shule ya kwanza hadi ya ishirini zimeainishwa kwenye Jedwali lifuatalo :

Ubora wa ufaulu wa shule umepangwa kwa kutumia kigezo cha “Grade Point Average” (GPA) kuanzia A = 1 hadi F = 5.  Shule zenye watahiniwa 40 na zaidi ziko 3,391. Shule ya kwanza hadi ya ishirini zimeainishwa kwenye Jedwali lifuatalo :

NAFASI
JINA LA SHULE
IDADI YA WATAHINIWA
MKOA
1
ST. FRANCIS GIRLS
90
MBEYA
2
MARIAN BOYS S.S
75
PWANI
3
FEZA BOYS S.S
69
DAR ES SALAAM
4
MARIAN GIRLS S.S
88
PWANI
5
ROSMINI  S S
78
TANGA
6
CANOSSA S.S
66
DAR ES SALAAM
7
JUDE MOSHONO S S
51
ARUSHA
8
ST. MARY’S  MAZINDE JUU
83
TANGA
9
ANWARITE GIRLS S S
49
KILIMANJARO
10
KIFUNGILO  GIRLS S S
86
TANGA
11
FEZA GIRLS
49
DAR ES SALAAM
12
KANDOTO SAYANSI GIRLS SS
124
KILIMANJARO
13
DON BOSCO SEMINARY SS
43
IRINGA
14
ST.JOSEPH MILLENIUM
133
DAR ES SALAAM
15
ST.JOSEPH’S ITERAMBOGO SS
64
KIGOMA
16
ST.JAMES SEMINARY SS
44
KILIMANJARO
17
MZUMBE SS
104
MOROGORO
18
KIBAHA SS
108
PWANI
19
NYEGEZI SEMINARY SS
68
MWANZA
20
TENGERU BOYS SS
76
ARUSHA
7.0        SHULE KUMI AMBAZO HAZIKUFANYA VIZURI ZAIDI KATIKA KUNDI LA SHULE ZENYE WATAHINIWA 40 AU ZAIDI

NAFASI
JINA LA SHULE
IDADI YA WATAHINIWA
MKOA
1
MIBUYUNI S.S
40
 LINDI
2
NDAME  S.S
41
UNGUJA
3
MAMNDIMKONGO S.S
63
PWANI
4
CHITEKETE S.S
57
MTWARA
5
MAENDELEO S.S
103
DAR ES SALAAM
6
KWAMNDOLWA S.S
89
TANGA
7
UNGULU S.S
62
MOROGORO
8
KIKALE S.S
60
PWANI
9
NKUMBA S.S
152
TANGA
10
TONGONI S.S
56
TANGA
8.0           TATHMINI YA UFAULU WA WATAHINIWA WA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE MWAKA 2012 
8.1           Tathmini ya awali iliyofanyika kuhusu ufaulu wa watahiniwa katika shule mbalimbali inaonesha kuwa shule zilizofanya vizuri zaidi ni zile ambazo zina mahitaji yote ya msingi ikiwemo walimu wa kutosha, miundombinu na vifaa vya kufundishia na kujifunzia.  Aidha, shule zenye ufaulu wa chini ni zile ambazo zina changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na:
(i)         Baadhi ya shule za vijijini hazina kabisa walimu wa masomo ya Sayansi na Hisabati na pia zina upungufu mkubwa wa walimu wa masomo mengine;
(ii)        Kutokuwepo kwa maabara kwa shule zenye mikondo ya sayansi na pia kutokuwepo kwa maktaba kwa ajili ya kujisomea; na
(iii)       Upungufu mkubwa wa vitabu vya kiada na ziada. Katika baadhi ya shule uwiano wa kitabu kwa mwanafunzi ni 1:10.
8.2           Mkakati wa Serikali ni kuendelea kupunguza changamoto hizo kila mwaka ikiwa ni pamoja na kufanya mambo yafuatayo:
(i)             Kuajiri walimu kila mwaka ili kuondoa upungufu uliopo katika shule zetu. Mwaka 2011/2012 Serikali iliajiri walimu wa sekodari 13,246 na mwaka huu wa fedha 2012/2013 imeajiri walimu 12,973 ambao wamepangwa katika shule zenye upungufu mkubwa wa walimu. Ajira ya walimu wapya mwaka huu umetuwezesha kuwa na wastani wa walimu 2-3 kwa shule.  Hali hii itaendelea kuboreka kadri tunavyoendela kuajiri walimu.
(ii)            Kuboresha miundombinu iliyoko katika shule zetu ikiwa ni pamoja na kujenga nyumba za walimu, madarasa na maabara. Mwaka 2012/2013 Serikali imepanga kuboresha miundombinu katika shule 264 zilizopo katika mazingira magumu ikiwemo miundombinu ya maabara na nyumba za walimu.
(iii)           Kuendelea kutoa ruzuku ya Tsh 25,000 kwa mwanafunzi kwa mwaka, ambapo asilimia 50 ya fedha hizo ni kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia ili kuziwezesha shule kununua vitabu pamoja na vifaa vingine muhimu kitaaluma.
(iv)           Wizara kuendelea kuzishauri Halmashauri kuweka mgawanyo mzuri wa walimu waliopo baina ya shule na shule.
(v)            Wizara itaendelea kuimarisha Idara ya Ukaguzi wa Shule pamoja na kuwawezesha Waratibu Elimu Kata na Wakuu wa Shule kufanya ukaguzi wa ndani katika Shule za Sekondari zilizo katika maeneo yao.

9.0           MATOKEO YA MITIHANI YALIYOZUIWA
Baraza la Mitihani la Tanzania limezuia kutoa matokeo ya:
(a)           Watahiniwa 28,582 wa Shule ambao hawajalipa ada ya Mtihani hadi watakapolipa ada wanayodaiwa pamoja na faini; na ikiwa hawatalipa katika kipindi cha miaka miwili (02) toka matokeo kutangazwa, matokeo yao yatafutwa.
(b)           Watahiniwa 65 wa kujitegemea na 71 waliofanya Mtihani wa Maarifa (QT) mwaka 2012 bila ya kulipa ada ya Mtihani hadi watakapolipa ada pamoja na faini. Ikiwa hawatalipa ada hiyo katika kipindi cha miaka miwili (02) toka matokeo kutangazwa, matokeo yao yatafutwa.

10.0        MATOKEO YA MITIHANI  YALIYOFUTWA
10.1              Matokeo Yaliyofutwa Kwa Sababu ya Udanganyifu
Jumla ya watahiniwa 789 wamefutiwa matokeo yao yote ya mtihani kwa mujibu wa kifungu Na.52(b) cha Kanuni za Mitihani baada ya kubainika kuwa walifanya udanganyifu katika mitihani ya Oktoba 2012. Kati yao, watahiniwa wa shule ni 624 na watahiniwa wa kujitegema ni 148 na watahiniwa wa Mtihani wa Maarifa (QT) ni 17.
Aina ya udanganyifu uliobainika na idadi ya watahiniwa husika ni kama ifuatavyo:
S/N
AINA YA UDANGANYIFU
IDADI YA WATAHINIWA
(i)        
Watahiniwa kubainika kuwa na skripti zenye miandiko tofauti au kuwa na miandiko tofauti katika skripti ya somo moja au zaidi ya moja.
04
(ii)       
Watahiniwa kukamatwa na wasimamizi ndani ya chumba cha mtihani wakiwa na ‘notes.’
170
(iii)      
Watahiniwa kubainika kuwa na mfanano usio wa kawaida wa majibu.
590
(iv)      
Watu kukamatwa wakiwafanyia watahiniwa wengine mtihani ‘impersonation”.
04
(v)       
Watahiniwa kukamatwa na simu ndani ya chumba cha mtihani.
06
(vi)      
Watahiniwa kukamatwa na wasimamizi wakibadilisha karatasi za maswali au skripti kwa lengo la kufanya udanganyifu.
15
JUMLA
789
10.2              Matokeo Yaliyofutwa Kwa Sababu ya Watahiniwa Kuandika Matusi Katika Skripti Zao
-----------
(i)          Jumla ya watahiniwa 24 waliandika matusi kwenye skripti zao za masomo mbalimbali. Kitendo hicho ni kosa kwa mujibu wa kifungu 5(13) cha Kanuni za Mitihani kinachosomeka:
“Written responses to any examination question which carry words, drawings or pictures connected to sex or abusive language in such a way that it becomes offensive shall consitute an examination offence and a candidate who commits such an offence shall be punished by the Council.”
Kutokana na kosa hilo Baraza la Mitihani limefuta matokeo  yao yote kwa mujibu wa Kifungu cha 6(2)(a) cha Kanuni za Mitihani kinachosomeka:  
“A candidate found to have committed an examination offence shall – (a) have his examination results nullified”
(ii)         Kitendo cha kuandika matusi kwenye karatasi za majibu (skripti) kinaonesha utovu wa nidhamu wa hali ya juu. Serikali haitaweza kuwavumilia hata kidogo watahiniwa wa aina hiyo. Hivyo, Serikali itaangalia hatua zaidi za kisheria za kuchukua dhidi ya watahiniwa wote walioandika matusi.
Kwa mujibu wa kifungu Na. 6(2)(b) cha Kanuni za Mitihani, watahiniwa wote waliobainika kufanya udanganyifu katika mitihani au kuandika matusi katika skripti zao hawataruhusiwa kufanya mitihani inayoendeshwa na Baraza la Mitihani la Tanzania  kwa kipindi cha mwaka mmoja (01) kuanzia tarehe ya kutangazwa kwa matokeo.

11.0        KUANGALIA MATOKEO YA MTIHANI WA CSEE na QT, 2012
(a)           Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) na Maarifa (QT), 2012  yanapatikana katika tovuti zifuatazo: 
·               www.matokeo.necta.go.tz,
·               www.necta.go.tz,     
·               www.udsm.edu.ac.tz, au
·               http://www.moe.go.tz
(b)           Matokeo yanaweza kupatikana pia kwa njia ya  ujumbe mfupi wa maneno (SMS) kwenda namba 15311. Jinsi ya kutuma ujumbe andika:
MATOKEOXNAMBA YA KITUOXNAMBA YA MTAHINIWA
(Mfano : matokeoxS0101x0503)

Dkt.  Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb)

WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

18 Februari 2013

KUPATA MATOKEO HAYO BOFYA HAPO CHINI
Posted by Unknown at 7:04 PM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
Newer Posts Older Posts Home
Subscribe to: Comments (Atom)

widgets
widgets

SPORTS NEWS

FOLOW ME ON TWITTER

Tweets by @ErickMalisa

CHECK ME IN INSTAGRAM

Instagram
Blogger Widgets

Popular Posts

  • Top five: Richest players in world football Cristiano Ronaldo, Lionel Messi & David Beckham are among the top five richest footballers
    Beckham is the world's richest footballer  (©GettyImages) The wages of football players is a fairly touchy subject, many arg...
  • Chris Bosh Wife 'Adrienne Bosh' Showing Off Her Bikini DONK On a Beach In Puerto Rico. WOW!! -- Photos Inside
    Chris Bosh Wife 'Adrienne Bosh' Showing Off Her Bikini DONK On a Beach In Puerto Rico. What Did Lil Wayne And Cameron Say?? lol -...
  • Lauren London Say Her BUTT All Natural 'No Butt Shots' + Lauren Talks New Movie Baggage Claim and Much More!
    Lauren London Say Her BUTT All Natural 'No Butt Shots' + Lauren Talks New Movie Baggage Claim and Much More! Lauren London...
  • SMOKING HOT: Beyonce Shows Off Her Bikini Body In New 'H&M Ad Campaign' And Swimsuit Line!! (Sexy) -- Video Inside
    SMOKING HOT: Beyonce Shows Off Her Bikini Body In New H&M Ad Campaign And Swimsuit Line!! -- Beyonce up’ed the hotness factor for her...
  • Jackie Robinson Biopic '42' Sets a Baseball Movie Record, Earning $27.3 Million Opening Weekend! Peep Out The Movie Review From The Shadow League.
    Jackie Robinson BioPic '42' Sets a Baseball Movie Record, earning $27.3 million Opening Weekend! Peep Out The Movie Review From T...
  • Watertown Shootout At MIT: What We Know So Far (PHOTOS)
    Shootings and chaos taking place at the campus of MIT as an officer loses his life after being shot multiple times. || Photo C...
  • Esther Baxter Instagram!!....Joe Budden Ex Girlfriend Esther Baxter Released New Sexy Photos On Instagram!!
    Esther Baxter Instagram!!....Joe Budden Ex Girlfriend Esther Baxter Released New Sexy Photos On Instagram!! -- Esther Baxter Instagram!!....
  • MNYIKA VS NAPE, FORM FOUR RESULTS NAPE NNAUYE
    MNYIKA VS NAPE, FORM FOUR RESULTS NAPE NNAUYE DIV IV-29 KISW D, HIST D, GEOG D, ENG F, B/MATH F, BIOL D, CHEM D, PHY D, CIV J...
  • Iggy Azalea Signs To 'Def Jam' No Longer Using Grand Hustle For Distributing Through Atlantic Records!! ( Hot Photos) -- Details Inside
    Iggy Azalea Signs To Def Jam, No Longer Using Grand Hustle Official Distribution Home Atlantic Records!! -- Iggy Azalea has inked a new ...
  • (no title)
    Jim Jones Boo 'Chrissy Lampkin' Butt Naked and Covered In Tattoos For Jimmy's Vampire Life Clothing!!  Jim Jones Boo ...

Total Pageviews

Followers

Blog Archive

  • ►  2012 (8)
    • ►  October (8)
  • ▼  2013 (336)
    • ▼  February (17)
      • Matokeo ya kidato cha Nne 2012
      •    Click Hapo chini uangalie moja kwa m...
      • NECTA yatangaza Matokeo ya Kidato cha Nne 2012 ...
      • HATIMAE WIZ KHALIFA NA AMBA ROSE WAPATA MWANA
      • Mchungaji Antony Lusekelo azungumzia Kuchinja!
      • Wanafunzi wajiua kwa matokeo kidato cha IV
      • Diamond Platnumz Azungumzia Kuhusu Mganga Aliyejit...
      • JCB Afunga Ndoa...
      • Kanisa katoliki laruhusu tembe za kuzuia mimba
      • Kanisa katoliki laruhusu tembe za kuzuia mimba
      • BEKI BLACK STARS (John Paintsil) AMEMSHAMBULIA MKE...
      • Patrice Muamba uanjani tena
      • MNYIKA VS NAPE, FORM FOUR RESULTS NAPE NNAUYE
      • DEMU MPYA WA DIAMOND WAMFANANISHA NA WEMA.
      • Zanzibar: Imamu wa msikiti auwawa kikatili!
      • Waraka wa Tatu wa Lema Kwa Rais Kikwete
      • CHADEMA: Kawambwa amebakiza siku kumi
    • ►  March (117)
    • ►  April (183)
    • ►  May (19)

Follow Me On Twitter

Blogger WidgetsBlogger Widgets

WATAZAMAJI


widget

WANTED

  • 2face (1)
  • A.J. Green (1)
  • Al Capone (1)
  • Alicia Keys (1)
  • Amber Rose (2)
  • Barack Obama (1)
  • Beyonce (1)
  • Big Sean (1)
  • Boston Bombing (4)
  • Brandy (1)
  • Cassie (1)
  • CHADEMA (1)
  • Chris Brown (1)
  • Chris Tucker (1)
  • Ciara (1)
  • Coolio (1)
  • Cristiano Ronaldo (2)
  • Damn Kanye (1)
  • David Beckham (1)
  • Donté Stallworth (1)
  • Draya Michele (1)
  • Erica Mena (2)
  • Esther Baxter (1)
  • Fancy (1)
  • Fantasia (1)
  • Fat Joe (1)
  • Flaviana Matata (1)
  • Floyd Mayweathe (1)
  • Frank Ski (1)
  • Halle Berry (2)
  • Iggy Azalea (1)
  • Interview (1)
  • J. Jackson (1)
  • Jada Pinkett (1)
  • Jaden (1)
  • Janet Jackson (1)
  • Jay-Z (6)
  • Jennifer Hudson (1)
  • Jim Jones (1)
  • Jobs (1)
  • JoJo Simmons (1)
  • JOSE MOURINHO (1)
  • Juanita Bynum (1)
  • KAJALA (1)
  • Kandi Burruss (1)
  • Kanye (1)
  • Kanye West (1)
  • Katt Williams (2)
  • Keith Hunnid (1)
  • Kelly Rowland (1)
  • Kevin Hart (2)
  • Keyshia Cole (1)
  • Kim Kardashian (1)
  • Kobe Bryant (3)
  • La Toya Jackson (1)
  • Lil Flip (1)
  • Lil Phat (1)
  • Lil Scrappy (2)
  • Lil Wayne (3)
  • Lindsay Lohan (1)
  • Links za kuangalia matokeo (1)
  • Lionel Messi (1)
  • LL Cool J (1)
  • LULU (1)
  • Manchester United (1)
  • Mariah Carey (1)
  • Mary (1)
  • Matt Clarke (1)
  • Maya Angelou (1)
  • Meagan (1)
  • Michael Clark (1)
  • Michael Clarke (1)
  • Michael Jackson (1)
  • Michael Jordan (1)
  • Mike Tyson (1)
  • Mona Scott (1)
  • NASA (1)
  • Nelly (1)
  • Nicki Minaj (1)
  • North Korean (1)
  • Oprah (1)
  • P Diddy (1)
  • PARIS HILTON (1)
  • Prince Sole (1)
  • Ramzez (1)
  • Ray J (1)
  • Rick Ross (5)
  • Rihanna (2)
  • Ryan Collins (1)
  • Serena Williams (1)
  • Sheree Whitfield (1)
  • Snoop Dogg (1)
  • Star Jones (1)
  • Steve Harvey (1)
  • T.I (2)
  • Taifa Stars (1)
  • Tamar Braxton (1)
  • Tiger Woods (1)
  • Uganda (1)
  • Usher (1)
  • Vanessa Williams (1)
  • Wesley Snipes (1)
  • Will Smith (1)
  • Wiz Khalifa (2)
  • Zitto (1)

VIVA MAN U

EPL TABLE

Erick Malisa ©2013 All Rights Reserved. Awesome Inc. theme. Powered by Blogger.